Monday, July 30, 2018

PETERPSQUARE AFUNGUKA CHANZO CHA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA PSQUARE

Imechukua muda kidogo toka kundi bora la muziki duniani ambalo lilikuwa linaundwa na mapacha wawili #PSQUARE kuvunjika hapo hakuna mmoja kati yao ambaye alijitokeza na kusema sababu hasa za undani za kuvunjika kwa kundi hilo.

Ila moja ya founder wa kundi hilo Peterpsquare amefunguka kwa mara ya kwanza juu ya sababu za kuvunjika kwa kundi hilo.

Well Peterpsquare amesema sababu kubwa kabisa ya kundi hilo kuvunjika ni kutokana na his twin brother Rudeboypsquare kushindwa kuiheshimu familia yake kwa maana mke wake na watoto pia.
 amesema ili kundi hilo lirudi lazima kwanza kila mmoja ajifunze kuheshimu familia ya mwenzake na amedai kwamba yeye hajawahi kuikosea heshima familia ya mwenzake ila mwenzake #PAUL amekuwa na tabia ya kumkosea heshima yeye pamoja na mke wake.
Amesema aliamua kujitoa kwenye kundi hilo kwa ajili ya kuilinda familia yake kwani alishaahidi kwamba atailinda familia yake kwa njia yoyote ile toka siku ya kwanza amepokea kiapo cha ndoa.
Amepata nafasi ya kuzungumza hayo alipokuwa akifanyiwa mahojiano na kituo cha Citizentvkenya.

Kwa upande mwingine msanii huyo ameonekana kwenye picha ya pamoja na msanii anayekimbiza kunako game ya bongofleva Benpol na kuzua maswali kwamba huenda kuna kazi inakuja baina ya wasanii hao wawili.

No comments:

Post a Comment