Sunday, August 26, 2018

HISTORIA YA OMMY DIMPOZ TANGU ALIPOINGIA KWENYE SANAA YA MUZIKI

Omary Faraji Nyembo (amezaliwa tar. 12 Septemba1987) ni jina la mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania ambaye anajulikana kwa jina la kisanii kama Ommy Dimpoz. Ommy alianza kusikika kwenye wimbo wa Utamu Iliyotoka 4/12/2012 alioshirikishwa na Dully Sykes, Lakini alianza kuvuma kwa wimbo wake wa Nai Nai iliyotoka 2/07/2014, aliomshirikisha Ali KibaBaadaye Iliyotoka 03/07/2014, Me and You Iliyotoka 2/07/2014, alioshirikishwa na Vanessa Mdee, Mama Iliyotoka 13/04/2015, alioshirikishwa na Christian Bella, Hello Baby alioshirikishwa na Avril kutoka KenyaCheche Iliyotoka 23/09/2017, Achia Body Iliyotoka19/12/2015, Tupogo iliyotoka 22/05/2014, Ndagushima Iliyotoka 16/05/2014, Wanjera Iliyotoka 12/03/2015, Kajiandae Iliyotoka 5/05/2016, Aliomshirikisha AliKiba Na Wimbo wake latest unaojulikana kama Yanje Iliyotoka 1/may/2018 aliomshirikisha msanii Seyi Shay kutoka nchini Naigeria.  Ommy Dimpoz ni msanii mwenye masihara na maneno mengi ya kuchekesha. Sawa na Rayvanny wa WCB. Ommy ni moja kati ya wasanii ambao wanajali sana faragha za maisha yao. Awali mwaka 2016 kulikuwa na gumzo kubwa baada ya Nay wa Mitego kumwimba vibaya Ommy kwenye wimbo wake na kumshutumu kama shoga. Baadaye Ommy akajibu kwa kuonesha picha ya mwanamke wake.[2] Ommy ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Pozi kwa Pozi Entertainment ambayo meneja wake (Mubenga) aliachia ngazi mwaka wa 2016.[3] Tangu wimbo wa Cheche (2017), amekuwa chini ya lebo ya Rockstar4000 ambayo iko chini ya Ali Kiba.
Mwaka 2018 umekuwa mbaya kwa msanii Ommy Dimpoz kutokana na ugonjwa wa koo unaomsumbiua sana na hatimae kupelekwa nchini south Afrika kwa matibabu. Ambapo alifanyiwa upasuaji na kuruhusiwa hivi karibuni tena amelirudishwa hospital kwa uangalizi Zaidi baada ya kusikika kwamba hali imezidi kuwa mbaya Zaidi. Ingawa wengine wamekuwa wakitoa taharifa ya kwamba amepelekwa chumba cha uangalizi maalumu inayojulikana kama ICU, lakini kwa upande wa mameneja wake wamekanusha na kusema taharifa hizo ni za uongo mkubwa.

No comments:

Post a Comment